Chuo cha Ualimu Morogoro kimefanikiwa kufanya uchaguzi wa Serikali ya Wanachuo kwa kupitia mtandao (Online Election System).
Mafanikio haya yamechochewa na uwepo wa vifaa na mifumo ya Tehama ambayo Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekua na mahusiano mazuri na mashirika binafsi ambayo yametoa msaada wa vifaa hivyo.
Shirika la Lyara in Africa lilifanikiwa kutuwezesha kupata vifaa vya tehama kama kompyuta 30, server pamoja na meza 30 kwa ajili ya kompyuta.